Hii ndo Story yenye wasee wengi hua hawaongelelei
“HELB imeingia!”
Hiyo ndio message Kevin alipost kwa WhatsApp group yao ya campus. Ndani ya masaa kiasi, alikuwa amesha-order nguo mpya, plans za weekend zilikuwa zimepangwa na kila kitu ilifeel kama life iko sorted. Kwa mara ya kwanza, alikuwa na pesa yake . No pressure, no accountability.
Na si Kevin tu . Campus nyingi, siku HELB inaingia huwa kama holiday. Watu wanatoka, wanasherehekea, wanabuy vitu walikuwa hawajawahi afford.
Hio moment huwanga Inafeel deserved.
Lakini hakuna mtu huongelea part 2 ya story.
Fast forward miaka mbili baadaye.
Hakuna story za “HELB imeingia.”
Hakuna allowance.
Hakuna soft life.
Ni emails za repayment.
Ni job applications full of disapointments.
Ni rent, food na pressure ya maisha.
Kevin sasa anakaa room akicheki tenje yake, akiona ile same message lakini this time ni kutoka Higher Education Loans Board, ikimkumbusha loan yake imeanza kumature.
Na hapo ndio reality inaingia.
Pesa ambayo ilionekana “kidogo na ya sherehe” campus, sasa inaonekana ilikuwa a rare chance. Chance ya kufanya better choices. Chance ya kujiandaa na maisha ya after.
Research na discussions mingi Kenya zinaonyesha kitu moja wazi: students wengi huwa hawaplan vile wanatumia HELB. Si kwa sababu eti wako careless but ni ju hakuna mtu aliwaonyesha impact ya kesho.
Na ukweli ni:
HELB si free money. Ni maisha yako ya baadaye, imeletwa mapema.
Story ya Kevin si unique. Ni story ya wengi. Na inaweza kuwa yako ama unaweza i-change.
Swali si kama HELB itaingia.
Swali ni: utaitumia aje?